Quantcast
Channel: MO BLOG » Admin
Viewing all articles
Browse latest Browse all 1758

Pinda atunuku vyeti na Diploma kwa Wahitimu wa Chuo cha Nyuki Tabora.

$
0
0

IMG_0745

Waziri Mkuu, Mizengo Pinda, Waziri wa Maliasili na Utalii, Hamisi Kagasheki (wa pili kulia), Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu, Uwekezaji na Uwezeshaji, Dr. Mary Nagu (kulia), Mkuu wa Mko a wa Tabora, Fatuma Mwasa (watatu kushoto ), Mbunge wa Tabora  Mjini Aden Rage (kushoto) na Mwenyekiti wa  Baraza  la Chuo cha Nyuki Tabora, Liana Hassan (watatu kulia)  wakiimba wimbo wa Taifa katika mahafali ya  Chuo cha Nyuki cha Tabora ambapo Mgeni rasmi alikuwa ni Waziri Mkuu Agosti  30, 2013. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu).

IMG_0841

Waziri Mkuu, Mizengo Pinda akiwaaga wahitimu wa Chuo cha Nyuki cha Tabora  baada ya kuwatunuku vyeti, Diploma  katika  mahafali ya Chuo hicho jana.

IMG_0660

Waziri Mkuu, Mizengo Pinda akitazama mizinga ya kisasa katika maonyesho ya Chuo cha Nyuki cha Tabora akiwa mgeni katika mahafali ya Chuo hicho  mjiniTabora Agosti 30, 2013. Wapili kushoto ni mwenyekiti wa Bodi ya Baraza la Chuo hicho, Liana Hassan.

IMG_0697

Waziri Mkuu, Mizengo Pinda akitazama baadhi ya vifaa vya kusindika asali katika maonyesho ya Chuo cha Nyuki cha Tabora  ambako alikuwa mgeni rasmi katika mahafali ya Chuo hicho. Kushoto ni Waziri  wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu, Uwezeshaji na Ukwekezaji, Dr. Mary Nagu na Wapili kushoto ni Mkuu wa Mkoa wa Tabora, Fatuma Mwasa na kushoto kwa Waziri Mkuu ni Mwenyekiti wa Bodi ya Baraza  la Chuo hicho, Liana Hassan.

IMG_0721

Waziri Mkuu, Mizengo Pinda akitazama baadhi ya vifaa vya kusindika asali katika maonyesho ya Chuo cha Nyuki cha Tabora  ambako alikuwa mgeni rasmi katika mahafali ya Chuo hicho. Kushoto ni Waziri  wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu, Uwezeshaji na Ukwekezaji, Dr. Mary Nagu.

IMG_0735

Waziri Mkuu, Mizengo Pinda akifungua  bwalo la chakula la Chuo cha Nyuki cha Tabora akiwa mgeni rasmi katika  Mahafali ya Chuo hicho jana.  Wapili kulia ni Waziri wa Maliasili na Utalii,Balozi  Hamisi Kagasheki  na kulia ni Mwenyekiti wa Baraza la Chuo hicho, Liana hassan na Watatu Kulia ni Mbunge wa Tabora Mjini, Aden Rage.


Viewing all articles
Browse latest Browse all 1758

Trending Articles