Katibu Mkuu wa Chama cha Mapinduzi Ndugu
Abdulrahman Kinana akisalimiana na Mkuu wa mkoa wa Mbeya Mh Abbas
Kandoro mara baada ya kuwasili katika ofisi za chama hicho mjini Viwawa
Wilaya ya Mbozi asubuhi hii akitokea wilaya ya Momba katika ziara
yake ya kikazi ya mikoa mitatu Ruvuma, Mbeya na Njombe, Kinana
ameongozana na ujumbe wake akiwa na Nape Nnauye Katibu wa NEC Itikadi,
Siasa na Uenezi na Dr. Asha Rose Migiro Katibu wa NEC Siasa na
Uhusiano wa Kimataifa.PICHA NA KIKOSI KAZI CHA
FULLSHANGWE-MBOZI Dr. Asha Rose Migiro Katibu wa NEC Siasa na
Uhusiano wa Kimataifa akisalimiana na mkuu wa mkoa wa Mbeya
Mh. Abbas Kandoro mara baada ya msafara wa Katibu Mkuu wa CCM ku
wasili mjini Vwawa wilayani Mbozi asubuhi hii, kushoto ni
Nape Nnauye Katibu wa NEC Itikadi, Siasa na
Uenezi Baadhi ya wana CCM wakishiriki kucheza
ngoma na kikundi cha ngoma kilichokuwa kikitumbuiza wakati wa mapokezi
ya katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana. Baadhi ya machifu wa Mbozi wakisubiri
kusalimiana na Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana.
Baadhi ya viongozi mbalimbali na wananchi
wakimlaki Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana
wakati alipowasili wilayani Mbozi. Mwenyekiti wa CCM mkoa wa Mbeya na mbunge
wa jimbo la Mbozi mashariki Ndugu Godfrey Zambi akisalimiana na wana
CCM wakati wa mapokezi hayo Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana
akisalimiana na machifu Wana CCM wakiwa katika mapokezi
hayo Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana
akifutrahia ngoma ya asili ya wanyiha iliyokuwa ikitumbuizwa katika
mapokezi hayo.
↧
Kinana awasili Viwawa wilayani Mbozi
↧