Mbunge wa Jimbo la Ubungo Mh. John Mnyika akizungumza na waandishi wa habari wakati akizindua rasmi taasisi aliyoiasisi ya “Ubungo Development Initiative-UDI” inayoendesha kampeni ya ‘Changia Maabara na Maktaba za Shule, ambapo amesema dira yake ni kuwa na jamii iliyoendelea yenye ushiriki mpana wa wananchi.(Picha na Geofrey Mwakibete wa Mo Blog).
Mh. Mnyika (kulia) akionyesha bango la kampeni ya Changia Maabara na Maktaba za Shule kuashiria kuzinduliwa kwa taasisi ya UDI.kushoto ni katibu Mtendaji -UDI John Mallaga.
Katibu Mtendaji wa “Ubungo Development Initiative-UDI” John Mallaga akifafanua jambo kwa waandishi wa habari wakati wa uzinduzi huo.
Mwenyekiti wa Kampeni ya kukuza Elimu inayoendeshwa na “Ubungo Development Initiative-UDI” Pascal Maziku, akielezea lengo la kampeni hiyo ambapo amesema ni kusaidia shule zilizopo katika jimbo la Ubungo kuwa na maabara za kisasa zenye vifaa na pia maktaba zenye vitabu ili kusaidia kukuza elimu, na kuwa dhima ya UDI ni kuhamasisha uwajibikaji na utoaji huduma bora.