Habari wadau, naomba kuwajulisha kuwa mwanachama mwenzetu wa TASWA, ambaye pia ni Makamu Mwenyekiti wa Chama cha Waaandishi wa Habari za Michezo Tanzania –TASWA Bw. Maulid Kitenge (pichani), amefiwa na baba yake mzazi Mzee Baraka Kitenge.
Msiba huo umetokea jana katika Hospitali ya Taifa ya Muhimbili.
Kwa mujibu wa Maulid ni kuwa msiba upo JET Lumo na maziko yanatarajiwa kufanyika leo Jumatano katika makaburi ya Kisutu jijini Dar es Salaam.
Kwa mawasiliano zaidi namba ya Maulid ni 0713-248740.
Mo Blog inatoa pole kwa mwanamichezo Mauled Kitenge, ndugu, jamaa, marafiki, watangazaji na wanamichezo wote kwa ujumla kwa msiba huo. Tunamuomba Mwenyezi Mungu awape nguvu na ujasiri katika kipindi hiki kigumu cha msiba.
“Inna Lillahi wa inna ilaihi raji’un”