Afisa Mipango Wilaya Kusini Unguja Bw. Faida Khamis Ali akifungua mafunzo ya siku tatu juu ya uelimishaji wa sheria ya uvuvi kwa wakuu wa madiko na wavuvi,katika skuli ya kitogani Kusini Unguja (kulia) Mratibu wa mradi Bw. Omar Muh’d na (kushoto) ni Makamo M/kiti wa Jumuiya maendeleo ya Wavuvi wa Kojani (KOFDO) Ussi Suleiman.
Mkufunzi Muhammed Kassim (alie simama kulia) akitoa elimu yuu sheria ya uvuvi ya Zanzibar katika mafunzo yaliyo fadhiliwa na the Foundation for Civil Society huko Kitogani Kusini Unguja.
Baadhi ya washiri wa mafunzo ya uelimishaji wa sheria ya uvuvi wakimsikiliza kwa makini Mkufunzi Muhammed Kassim (hayupo pichani) katika mafunzo juu ya sheria ya uvuvi.
Mshika Fedha wa Jumuiya maendeleo ya Wavuvi wa Kojani (KOFDO) Faki Othman akichangia katika mafunzo ya sheria ya uvuvi huko Kitogani Kusini Unguja.(Picha na Makame Mshenga-Maelezo Zanzibar).