Basi la Kampuni ya Mtei Express liliokuwa likifanya Safari zake Singida – Arusha lenye namba za usajili T742 ACU limeua watoto watatu wa familia moja waliokuwa wamepakizwa kwenye pikipiki na baba yao mzazi ambaye yuko mahututi baada ya kupasuka kichwa, ajali hiyo imetokea kwenye kijiji cha Kititimo mkoani Singida.
Wananchi wenye hasira kali wameamua kulipiga moto basi hilo pamoja na mizigo yake huku abiria wake wakiwa wamesalimika.
Hii ni taarifa fupi iliyotufikia hivi punde kutoka kwa mwakilishi wa MOblog Nathaniel Limu wa mkoani Singida aliyepo eneo la tukio. Pichani ni mmoja ya mabasi ya kampuni ya Mtei Express.
Habari zaidi na picha ni hapo baadae.