Quantcast
Channel: MO BLOG » Admin
Viewing all articles
Browse latest Browse all 1758

Kiongozi Mkuu wa kundi la waasi nchini Burundi akusudia kujitokeza hadharani baada ya kujificha kwa miaka mitatu.

$
0
0

agathon Rwassa

Kiongozi  wa  kihistoria  wa   kundi  la upinzani  nchini  Burundi Agathon Rwasa , anakusudia kujitokeza  hadharani  kwa mara  ya  kwanza  katika  muda  wa  miaka  mitatu na  kutangaza  mipango  yake  ya  kugombea  kiti  cha urais  katika  uchaguzi  wa  mwaka  2015.

Kiongozi  wa  kundi  la  zamani  la  waasi  la  National Liberation Forces (FNL) alikimbia  kutoka  Burundi  na kwenda  kuishi  mafichoni  baada  ya yeye  pamoja  na upinzani  nchini  humo  kupinga  uchaguzi  wa  mwaka 2010  kuwa  ulikuwa  wa  udanganyifu.

Serikali  ya  nchi  hiyo  ilimuona  kuwa  kitisho  tangu wakati  huo,  lakini  Rwasa  amerejea  mjini  Bujumbura siku  chache  zilizopita baada  ya kupata  uhakikisho kuhusu  usalama  wake.

Msemaji  wake  Aime  Magera  amesema  kuwa  Rwasa mwenye  umri  wa  miaka  49 anatarajiwa  kujitokeza hadharani  mbele  ya  wafuasia  wake pamoja  na  maafisa  wengine  mashuhuri, ikiwa  ni  pamoja na  wanadiplomasia  wa  mataifa  ya  kigeni.

Hakufahamika yuko  wapi  tangu  wakati  huo, ambapo  mara  kadhaa aliripotiwa  kuonekana  katika  nchi  za  jirani  katika  eneo la  Kivu  ya  kusini  katika  jamhuri  ya  kidemokrasi  ya Congo, pamoja  na  Tanzania  na  Zambia.


Viewing all articles
Browse latest Browse all 1758

Latest Images

Trending Articles



Latest Images